Leo ukiongelea makampuni ambayo yana thamani kubwa katika soko kwa sasa huwezi kuacha kuitaja Facebook. Hii imetokea baada ya kampuni hiyo kufikisha thamani ya dola trilioni moja za kimarekani.
Thamani yake kabisa kwa sasa ambayo imeripotiwa na mtandao wa yahoo uliojikita katika maswala ya fedha imeripotiwa kwamba ni kiasi cha dola trilioni 1.008 za kimarekani.
Ikumbukwe kuwa kampuni hilo linamiliki makampuni mengie kama vile Facebook yenyewe, WhatsApp, Instagram na Oculus ambayo yote kwa pamoja ukijumuisha ndio yanakuja kuipa Facebook thamani hiyo.
Facebook ilianzishwa rasmi miaka ya elfu mbili na dhamira yake kubwa ikiwa ni kutaka kuunganisha watu pamoja kwa kurahisisha mawasiliano baina ya mtu na mtu.
Mwaka huu umekua ni mzuri sana kwa makampuni ya kiteknolojia maana mengi yanapanda thamani yake katika soko.
Soma Makampuni Mengine Yaliyopanda Thamani —–> Hapa <—–
No Comment! Be the first one.