Ni wazi kwamba mtandao wa kijamii wa Instagram kwa sasa hauruhusu kupost picha na video kama ukiwa unatumia mtanda huo kwa kutumia kompyuta.
Hii yote itabadilika maana Instagram wenyewe wanafanyia majaribio kipengele hicho na kwa sasa wapo katika hatua za mwisho.
Achana na hii makala ambayo niliandika mwaka 2016 ambayo inahusiana sana na jambo hili, japo hii haikuwa moja kwa moja kutoka kwa instagram wenyewe.
Kipengele cha kuweza kupost ndani ya mtandao wa instagram kimekua kikisubiriwa kwa hamu na wengi na kupitia mtandao wa Twitter taarifa kuhusiana na ujui wa kipengele hicho ilishamiri.
More screenshots of creating + publishing posts via https://t.co/3QaHTLlqBE pic.twitter.com/G5mptOhN06
— Matt Navarra (@MattNavarra) June 24, 2021
Hili ni jambo zuri kutoka mtandoa wa instagram maana kwa muda tuu watumiaji wa mtandao huo waliomba uwezo huu uwepo ukiachana na kuweza ku’like na ku’comment post ambazo tayari zipo.
No Comment! Be the first one.