Facebook imebadili jina na kuitwa ‘Meta’, uamuzi huu ulifanyika ili kutoa nafasi kwa kampuni hii kuweza kuwekeza katika teknolojia zingine. “Kampuni yetu imeshikamana sana na huduma moja kiasi kwamba haiwezi kuwakilisha kila kitu tunachofanya leo, ukiachilia mbali katika siku zijazo,” Zuckerberg alisema.
Katika mpangilio huu mpya mitandao yote ya kijamii inayomilikiwa na Facebook kama Facebook, Instagram na Whatsapp pamoja na kampuni zingine zitakuwa chini ya Meta. Uamuzi huu wa kuweka kampuni mama kwaajili ya kusimamia kampuni zingine ulifanywa pia na Google mwaka 2015 ambapo Google iliunda kampuni mama inayoitwa Alphabet ili kusimamia shughuli zake zote pamoja na makampuni yake mengine.
Mmiliki wa Facebook alitangaza jina hilo jipya alipokuwa akizindua mipango ya kujenga “metaverse” – ulimwengu wa mtandaoni ambapo watu wataweza kucheza magemu, kufanya kazi na kuwasiliana katika mazingira ya mtandaoni. Mabadiliko mengine ya jina la kampuni yatatokea kwenye soko la hisa ambapo jina wakilishi litabadilika kutoka FB na kuwa MVRS mwishoni mwa mwaka huu.
Sababu zilizopelekea kampuni ya Facebook kubadili jina ni pamoja na kufululiza kwa malalamiko mbalimbali yanayohusu mtandao wa kijamii wa Facebook pamoja na Instagram kupuuzia habari potofu na maudhui hatarishi zinazosambaa katika majukwa yake.
No Comment! Be the first one.