Kuna mabadiliko ya vifurushi kwenye mtandao wa Tigo ambayo yameleta malalamiko mengi kutokana na kuwa ya makubwa katika ushushwaji wa viwango vya GB ambavyo mtu anapata kwa malipo ya kwa siku, wiki na mwezi.
Tigo hawatatoa maelezo yeyote kuelezea sababu ya mabadiliko haya ya vifurushi lakini ni mabadiliko makubwa sana ya bei na thamani ya GBs ambazo mtu anazipata anapolipia.
Kwa mfano ni siku chache tu nyuma nilijiunga kifurushi cha mwezi kwa gharama ya shilingi 20,000/= na nilipata GB 16 za kuweza kutumia kwa kipindi cha siku 30. Je shilingi 20,000 inakupatia GBs ngapi sasa kwa ajili ya kipindi hicho hicho cha mwezi? – GB 9. Kwa punguzo la GB 7 hii ina maanisha ni punguzo la gbs la kwa zaidi ya asilimia 40.
Kutoka 2,000/= kukupa 2.5GB hadi kukupa 1GB kwa siku.
Vifurushi vipya
Kwa muda mrefu huwa tunategemea mabadiliko makubwa ya gharama za maongezi na bidhaa nyingine mbalimbali katika kipindi cha bajeti za kiserikali au kukiwa na taarifa za aina mpya za tozo dhidi ya mitandao ya simu.
Je mabadiliko haya ya gharama za huduma ya intaneti kutoka Tigo yatakuwa yamesababishwa na nini? Tutaendelea kufuatilia lakini kama jambo ni la uhakika ni kwamba watanzania wengi wanamiliki laini zaidi ya moja na uamuzi huu wa Tigo unaweza sababisha wakapoteza wateja wengi kwenye huduma ya intaneti na kujikuta katika hali ya kufanya mabadiliko tena ya vifurushi hivi.
No Comment! Be the first one.