Baada ya Cambridge Analytica kugundulika kutumia taarifa za watu kwenye Facebook mengi yameibuka baada ya taarifa hiyo na sasa kampeni maalum ya kuwashawishi watu kuacha kutumia Facebook imeanza kama mwarobaini wa wao kuwa salama mtandaoni.
Kampeni hiyo ya #DeleteFacebook iliyoanzishwa na mwanzilishi mwenza wa WhatsApp, Bw. Brian Acton amekuwa mstari wa mbele kuhusu kampeni hiyo kwa kuwaambia watu ‘Waliomfuata’ kwenye ukurasa wake wa Twitter baada ya taarifa kuhusu Cambridge Analytica kutumia taarifa za watu kutoka Facebook.
Hatua hiyo ya kushawishi watu wafute akaunti zao za Facebook imekuaja baada ya Cambridge Analytica kutumia taarifa za watu (kwenye Facebook) takribani 50mil bila idhini yao.
Kitendo cha Cambridge Analytica kututumia taarifa za watu kutoka Facebook kimefanya mamlaka husika za Uingereza na Marekani kufikiria kuchunguza iwapo taarifa watu watu kutoka mataifa hayo mawili nazo zilichukuliwa bila idhini kutoka kwa wahusika.
Afrika nayo imekubwa na mkono wa Cambridge Analytica, nchini Kenya tayari wabunge wameomba uchunguzi ufanyike kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2017 iwapo kampuni hiyo ilihusika kumsaidia rais Uhuru Kenyatta kushinda katika uchaguzi huo.
Je, unafikiri ukifuta akaunti yako ya Facebook ndio itakuwa suluhisho la taaarifa za watu kutumiwa bila idhini? Tupe maoni yako.
Vyanzo: Gadgets 360, The Times of India
6 Comments
Comments are closed.