Katika ulimwengu mawasiliano kupitia vifaa vya kiganjani unapamba moto siku hadi siku kitu ambacho wengi wetu tumekuwa tukitumia WhatsApp kwa kiasi kikubwa tuu; pengine hata kuishia kuweka kifurushi cha intaneti pekee.
Tangu kuanza kutumia kwa WhatsApp Mei 3 2009 hadi leo hii maboresho mengi sana ambayo yamewekwa kwenye programu tumishi husika na kufanya ivutie zaidi lakini tukizungumzia suala zima la faragha ndio linazidi kuwa murua kweli.
Unaweza ukawa ni mmojawapo kati ya watu wengi wanaopenda “Ukimya kwenye WhatsApp” kwa maana ya kwamba jumbe nyingi tuu umeziamuru kuweza kuzifikia bila ya wewe kupata taarifa au kujulishwa ingawa bila sauti kutoka.
Sasa ni vyema ukafahamu kuwa kulingana na toleo la 2.20.197.3 kwenye WhatsApp Beta mtumiaji anaweza akaamuru daima asiweze kusikia sauti ya ujumbe unapoingia kutoka kwa mtu ama kundi/vikundi.
VIlevile, WhatsApp wanaonekana kurudisha machoni pa watu kipengele cha jumbe kuweza kufutika baada ya muda fulani kupita (siku 7) na hii ni kwa mujibu wa WABetaInfo ikionyesha mtu anaweza kukiruhusu au kutokukiruhusu kufanya kazi yake.
Hiyo ndio WhatsApp Beta na ukimya kwenye WhatsApp ambapo watumiaji wake wanapata kupokea masasisho kabla ya wengine wote. Vipi wewe msomaji wetu una neno la kusema kuhusu maboresho hayo?
Vyanzo: Gadgets 360, WABetaInfo
One Comment
Comments are closed.