Moto G30 ni simu janja ambayo inafaa wale wote ambao wanapenda rununu ambazo si zenye uwezo sana lakini zinaweza kutimiza kazi zake kikamilifu.
Moto G30 ina miezi kadhaa tangu kuzinduliwa kwake na kimsingi simu hii imelenga watu wenye uwezo wa kati hasa ukizingatia sifa za rununu husika Kiujumla simu hii haina sifa nyingi ambazo zinang’arisha vipengele mbalimbali ndani ya simu husika. Sifa za simu hii ni kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.5
- Ubora: IPS LCD (720*1600px, 90Hz); ina ung’avu wa kawaida tuu kutokana na aina ya kioo kilichowekwa
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4/6
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 8, 2 na 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 13+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W/20W
Kipuri mama :
- Snapdragon 662
Uzito :
- Gramu 200
Programu Endeshi
- Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi na Udhurungi
- Gharama yake inaanzia $219 (zaidi ya Tsh. 503,700) bei ya ughaibuni.
Simu hii pia ina toleo la Marekani ambapo tofauti na hiyo hapo juu ni kwenye memori (RAM-GB 4 na diski uhifadhi-64GB). Simu hii tayari imeshaingia sokoni kwa toleo la Marekani yenyewe itaanza kuuzwa Julai 30.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.