Kwa miaka kadhaa sasa simu janja za Nokia zimekuwa kwenye ulingo wa ushindani na makampuni mengine ambayo nayo yanatoa rununu zinazovutia na zinazoendana na teknolojia ya kusasa. Nokia G21 imezinduliwa leo ikiwa imeboreshwa maeneo mbalimbali.
Simu janja hii ambayo imezinduliwa leo ni kuboresha toleo lililopita kwa maana ya Nokia G20 ambapo kimsingi kuna maeneo mahususi ambayo HMD Global imeyalenga kwenye toleo hili jipya la simu janja. Maeneo hayo ni upande wa betri, kioo na kamera. Na huu ndio undani wa simu janja Nokia G21.
Muonekano|Kipuri mama
Hili ni eneo mojawapo ambalo Nokia G21 inajitofautisha na mtangulizi wake; kioo cha kwenye simu hii ni cha LCD (90Hz), kina urefu wa inchi 6.5. Hii inakuwa simu janja ya kwanza za Nokia kutoka kwenye familia ya “G” kuwa na uwezo wa kutoa ung’avu wa mpaka 90Hz. Simu hii inatumia Helio G35 kama kipuri mama.
Memori|Kamera
Hili ni eneo la pili ambalo simu hii inajivunia. Hapa utakutanana kamera kuu yenye MP 50 (G20 ina 48MP), kamera nyingine mbili zote zina MP 2. Kamera ya mbele ina MP 8. Kwa upande wa memori simu hii ina RAM GB kwa diski uhifadhi 64 GB au 128GB huku mtu akiwana uwezo wa kuongeza memori ya ziada.
Betri|Mengineyo
Eneo la tatu la na la mwisho la kuifanya simu hii kuwa ya kitofauti ukilinganisha na toleo lililopita ni eneo la betri ambayo ina 5050mAh ambayo inadumu na chaji kwa siku 3 mfululizo lakini ili hilo liwezekane ni muhimu kuwasha kipengele cha “Adaptive mode” ambacho kitapunguza ungávu wa muonekano kwenye kioo kutoka 90Hz hadi 60Hz. Mbali na hilo ina teknolojia ya kuchaji haraka kwa 18W.
Simu hii ipo tayari kupokea Android 12 na HMD Global wameweka wazi kuwa itapeleka Android 12 na 13 tu kwenye rununu husika pamoja na miaka mitatu ya masasisho ya kuifanya simu janja kuwa salama ambayo hutolewa hadi mara mbili kwa mwezi.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.