Tangia iPhone 12 Pro ilivyotoka ndio simu ya kwanza kutoka Apple ambayo imekuja na teknolojia ya LiDAR, tumeona vipengele vingi vipya kuja na hii ikiwa ni kama sehemu ya Apple kuboresha zaidi simu zao.
Kwa ulimwengu wa simu ilikua ni kitu kipya, na maswali yamekuwa ni mengi sana juu ya teknolojia hiyo na ufanyaji wake wa kazi. Kirefu cha LiDAR ni ‘Light Detection and Ranging’,
Teknolojia ya LiDAR ipo toka zamani japokuwa katika simu imekuja juzi juzi tuu! Kwa haraka haraka teknolojia hii inafanya kazi hivi; ni kwamba sensa inatoa miale (kama ile ya ‘infrared) mpaka kwenye kitu/umbo alafu miale hiyo inarudi katika sensa ikiwa na taarifa kamili za kitu/umbo hilo (mfano, ukubwa na upana).
LiDAR inapatikana katika kamera za iPhone 12 Pro, pengine itaendelea kupatikana katika simu zingine ambazo zitatokaa kama matoleo ya mbele kwa iPhone 12.
Teknolojia hii katika iPhone 12 Pro haina utofauti sana wa ufanyaji kazi maana ipo kama teknolojia ile ya ‘Face ID’ tofauti kubwa inakuwa ni umbali tuu ndio unatofautiana, kwa ‘Face ID’ inafanya kazi sura ikiwa karibu zaidi.
Kingine kizuri kutokana na LiDAR ni kwamba picha za mfumo wa ‘Portrait’ zinakuwa na uhalisia zaidi ukilinganisha na iPhone ambazo hazina teknolojia hiyo kama vile iPhone 11 na matoleo mingine ya nyuma.
Teknolojia hii inatumika kwa kisai kikubwa katika magari yanayojiendesha yenyewe. Ukiachana na magari, kwa sababu teknolojia hii inaboresha sana eneo la kamera ya simu kuna vitu vingi sana vimebadilika hata App ambazo zinahitaji matumizi ya kamera ili zifanye kazi zinafanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Fikiria kama App ya vipimo (measure) katika iPhone itaweza kutoa vipimo sahihi kulinganisha na matoleo ya nyuma ya simu ambazo hazina teknolojia hii.
Kuna michezo (games) ambayo kwa kiasi kikubwa inatumia kamera kwa mfano kama Pokemon Go kwa kutumia kamera ambayo ina teknolojia hii ya LiDAR utaweza kulifahidi zaidi.
Kwa sasa teknolojia hii inapatikana katika iPhone 12 Pro (zote) na iPad Pro tuu
Niambie hapo chini katika boksi la maoni, hii umeipokeaje? je unahisi ni teknolojia sahihi kuwepo katika kamera ya simu kwa kipindi hichi?
Tembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.