Katika simu ambazo bei yake hazishuki kwa wale ambao tunapenda “Simu ndogo” na zenye kutunza chaji muda mrefu hakika tunafahamu umaarufu wa Nokia 105.
Miaka miwili baadae HMD Global wameona ni wakati sahihi wa kutoa simu mbili bora zaidi ya watangulizi wake hapa naongelea Nokia 105 na 110 zote zikiwa na 4G nakini pia zikiwa na kwenda mbali kidogo mpaka kwenye “LTE”. Sifa zao nyinginezo bi kama ifuatavyo:-
Muonekano|Mawasiliano
Hapa simu zote mbili zina kioo chenye urefu wa inchi 1.8 ambapo kwa upande wa kufanya mawasiliano bidhaa hizi zimewezeshwa mawasiliano kwa njia ya sauti katika ubora wa 4G na hata LTE. halikadhalika toleo hili zipo ambazo zinatumia kadi moja ya simu na nyingine mbili.
Memori|Redio
Nokia 110 4G inavutia kwa namna yake kwa maana ya kwamba kwanza ina kamera lakini pia kuna sehemu ya kuweka memori ya ziada mpak GB 32 ambayo inaweza kutumia kuhifadhi vitu vingi tuu. Kwa upande wa redio wamezesha simu zote kuweza kuwasha redio bila kuhihitaji spika za masikioni ziazotumia waya.
Uwezo wa betri|Mengineyo
Simu zote mbili zina betri yenye 1020mAh ambayo inawezesha saa 5 za kuongea moja kwa moja, saa 16 zikitumika katika mfumo wa 2G, ina tochi mahususi kwa ajili ya kuleta mwangaza sehemu za gizani, zote zina sehemu ya kuchomeka spika za masikioni. Nokia 105 4G ni Nyekundu, Bluu na Nyeusi huku Nokia 110 4G inapatikana kwa rangi ya Bluu bahari mpauko, Nyeusi na Njano.
Bei zake bado hazijajulikana lakini kama zilizotangulia zile “Bei zake” tunazijua basi hizi tutegemee zitakwenda juu kidogo lakini pia itategemeana na mapokezi yake sokoni.
Vyanzo: GSMArena, Gizmochina
One Comment