Biashara ya simu janja kwa upande wa Nokia imeendelea kushamiri ambapo Nokia G20 imetoka ikiwa imewekwa mengi ya ambayo yanafanya kuiweka kampuni hiyo kwenye ushindani.
Kwa miaka mingi tuu nimekuwa mpenzi wa simu janja za Nokia na tangu warudi kwenye ushindani wa soko la ushindani wamekuwa wakiuza zaidi ya rununu milioni 11. Nokia G20 ni simu janja ambayo imeingia sokoni na sifa zake zinavutia kulingana na mahitaji ya teknolojia ya leo. Sifa zake ni:
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.52
- Ubora: IPS LCD (720*1600px); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 48, 5, 2 na 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 8+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5050 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 10W
Kipuri mama :
Mimi nimeinunua hii Nokia G20 lakini camera yake inatoa picha mbovu kuliko Nokia 3.1 niliyokuwa natumia kabla hasa camera yake ya selfie
Ulinunua mpya au kwa mtu?