Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amewaonya watu waliopewa dhamana ya kusimamia mifumo ya TEHAMA serikalini kutowakwaza Watanzania kwa kisingizio kuwa mitandao haiko vizuri.
Akizungumza katika uzinduzi wa mifumo ya Tehama serikalini jijini Dodoma, Majaliwa aliwaagiza watendaji, wakuu wa taasisi za umma, wataalamu kusimamia mifumo hiyo vyema ili iweze kutoa tija kwa watanzania.
Mifumo hii isitumike kukwamisha watu, shughuli za serikali kwa sababu ni teknolojia, wasiwakwaze wananchi kwa kuwaambia kwamba mtandao umeshuka~Mhe. Kassim Majaliwa. Aliwataka wananchi kutumia mifumo hiyo kwa sababu haina urasimu na wala hawatadaiwa rushwa katika utoaji wa huduma.
Wakati huo huo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Atashasta Ndetiye alisema kwa kushirikiana na wadau wanakamilisha uandaaji wa Mkakati wa Taifa wa Usalama wa Mtandao wa mwaka 2018.