Kampuni ya Bakhresa Group imetangaza ujio wa kampuni yake mpya ya kutoa huduma za mawasiliano ya simu pamoja na Intaneti.
Kampuni hiyo ya mawasiliano itajulikana kwa jina la Azam Telecom (T) Limited na tayari wameshapata kibali kutoka katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Amesema Azam Telecom (T) LTD ni moja makampuni tanzu ya bakhresa Group na kampuni hii imeanzishwa kwa lengo la kutoa huduma za kisasa kabisa za mawasiliano na kwa ubora wa hali ya juu na kwa gharama nafuu.