Kijana mmoja mwenye umri wa miaka 24, Brian Gitta, raia wa Uganda ameshinda zawadi ya mvumbuzi bora inayotolewa kila mwaka na Chuo cha taaluma ya Uhandisi (Royal Academy of Engineering Africa prize) cha nchini Uingereza.
Brian Gitta amepata tuzo hiyo baada ya kuunda kifaa kwa ajili ya kupima na kutambua ugonjwa wa malaria bila ya kutumia damu ya mgonjwa kama ilivyo desturi ya maabara.
Gitta pamoja na wenzake, wametengeza kifaa kidogo ambacho hakiihitaji utaalam katika kukitumia ambapo chenyewe humhitaji mgonjwa kukiweka kwenye kidole chake.
Kwa namna kilivyotengenezwa hutambua mabadiliko ya maumbo, rangi pamoja na wingi wa chembe hai nyekundu za damu ambazo zimeathirika kwa malaria. Majibu yanapatikana ndani ya dakika moja kupitia simu ya mkononi inayounganishwa na kifaa hicho.
Lakini Gitta na timu yake wamekuwa wakiboresha kifaa hicho na wana uhakika kwamba majaribio mapya yatakuwa ni majibu sahihi kwa asilimia 90 ya kutambua ugonjwa wa malaria.
Kufanyia majaribio ya kifaa hicho wanashirikiana na hospitali za kidhaa nchini Uganda. Lengo kubwa likwa ni kuwezesha Mattibabu kupatikana kwa watu binafsi, maabara, vituo vya afya na hospitalini.
Kupitia tuzo hizo watafiti wa kimataifa watakifanyia majaribio kifaa hicho na kutoa ripoti mwezi ujao kuhusu uwezo wa ‘Mattibabu’ katika kubaini mgonjwa anasumbuliwa na malaria.