Samsung imekuwa ikifanya uzinduzi wa bidhaa zake kwa miaka mingi tuu na shughuli hii huwekwa katika makundi; iwapo ni mkubwa au midogo na hii huwa inaaangalia vigezo kadha wa kadha.
Februari 9 ya mwaka huu Samsung wanatazamiwa kuzindua bidhaa zao mbalimbali na mitandao mingi imekuwa ikiongelea kuhusu uzinduzi ambaokampuni hiyo inatarajia kuufanya hivi karibuni. Si watu wengi ambao wanafahamu bidhaa zinazotarajiwa kuzinduliwa siku hiyo. Inaaminika Samsung watazindua:
Galaxy S22 na S22+
Kama walivyofanya mwaka 2021 walipotoa S22 Ultra na nduguze inaaminika pia katika uzinduzi huo ambao utafanyika siku za usoni tutapata kuziona toleo la Galaxy S22 na S22+ huku ikielezwa kufanana kwa karibu kabisa na S21 lakini ia kamera kuu yenye MP 50. Simu hizi zitatoka zikiwa na vipuri mama tofauti kulingana na soko; Zitakazouzwa Amerika Kaskazini (Marekani na Canada) zitakuwa na Snapdragon 8 Gen 1 halafu bara la Ulaya zitakuwa na Exynos 2200.
Galaxy S22 Ultra
Ni moja ya simu janja zilizosifisiwa kwa kiwango cha juu na Rais wa Samsung, Bw. TM Roh na kutokana na changamoto mbalimbali za mwaka 2021 zilizoathiri uzalishaji ilisababisha kuruka kuzindua simu za kutoka famili ya “Note”. Mwaka huu simu hizo zinarejea ikitazamiwa ndio itakuwa ndugu yake na Note 20 halikahalika kuwa na muundo wa tofauti kabisa na rununu nyingine za Galaxy S22.
Galaxy Tab S8 na Tab S8 Ultra
Bidhaa nyingine ambayo inatazamia kuzinduliwa Feb 9 ni tabiti ambazo miaka kadhaa nyuma Samsung walitangaza kuachana na utengnenzaji wa tabiti lakini karibuni wakaweka wazi kuwa watatoa tabiti bora ambazo zitakuwa ni “Komyputa zijazo”. Habari za chini zinasema tabiti S8 ina kioo cha inchi 11, kipuri mama-Snapdragon 8 Gen 1, betri-8000mAh, RAM GB 8/256GB za diski uhifadhi.
Mengi na ya uhakika kabisa tutapata kuyafahamu siku hiyo (Feb 9) ya uzinduzi. Tukusihi kusalia nasi ili kuweza kufahamu hicho ambacho kitafanyika siku hiyo.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.