Katika miezi ya karibuni WhatsApp ya kompyuta imekuwa ikiboreshwa na kuweza kufanana kwa karibu kabisa ina ile ya kwenye simu zetu kitu ambacho kwa wale ambao tunaitumia hakika tunaifurahia.
Mimi ni mtumiaji mzuri tuu wa WhatsApp ya kompyuta ambayo imekuwa ikinisaidia katika shughuli zangu za kila siku hasa ukizingatia natumia muda mwingi kuwa karibu na kipakatalishi. Sote ambao tunatumia huduma hii kupitia kwenye kivinjari au kwa kupakua programu mahususi inawekwa ndani ya ngamizi tunafahamu vyema kuwa siku hizi hatutegemei sana simu zetu ili kuweza kutumia WhatsApp.
Mbali na hilo pia kwenye WhatsApp ya kompyuta mtumiaji anaweza kurekodi/kusimamisha na kisha akaendelea ikiwa ni maboresho ya karibuni kabisa kuletwa. Sasa hivi sasa tena kwa watumiaji wote wa WhatsApp kupitia kwenye kivinjari/programu mahususi ya kompyuta wanaweza kusikiliza jumbe za sauti huku wakiwa na uwezo wa kutoka na kuendelea kuperuzi ndani ya WhatsApp.
Uwezo wa kusikiliza jumbe za sauti huku mtu akifanya mambo mengine ndani ya WhatsApp ni kitu ambacho kilikuwa kinawezekana kwa wale ambao wanaoitumia kupitia kwenye programu tumishi lakini kitu hicho sasa kimefika kwa watumiaji wengine.
Mpaka hapa toleo hili la programu hii yenye watumiaji wengi zaidi duniani imeendelea kufanya isionekane tofauti kubwa kati ya ile ya kwenye simu na hii ambayo inatumika kupitia kipakatalishi ama kivinjari. Wewe je, unatumia ipi mara kwa mara?
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.