WhatsApp Web ni maarufu kwa watu wengi tuu duniani kote na hii inatokana na kuwa mbadala wa simu janja katika kumfanya mtumiaji aweze kutuma/kupokea ujumbe kupitia tovuti/kompyuta.
Binafsi ni mtumiaji mzuri tuu wa WhatsApp Web na hivi karibuni nimehamia kwenye toleo la Beta ambalo limenivutia sana. KImsingi hapo awali ililazimu simu janja yangu kuwa kwenye intaneti ili kuweza kupokea/kutuma ujumbe kupitia WhatsApp kwenye kompyuta lakini mambo yamebadilika ama kwa lugha rahisi naweza kusema vitu vimeboreshwa!.
Kwa zaidi ya mwezi sasa sihitaji kuunganisha simu yangu kwenye intaneti ili kuweza kufanya mawasiliano na watu kwenye WhatsApp kwa kutumia kompyuta; toleo la WhatsApp Web Beta limebadiulisha mambo ambapo mtu anaweza kuunganisha vivinjari hadi vinne(4) kwa namba ileile kuweza kuwasiliana kwenye WhatsApp BILA KUTEGEMEA SIMU JANJA.
Je, kitu hiki kinawezekanaje?
Kwanza kabisa ni lazima mtumiaji awe anatumia WhatsApp Web toleo la majaribio (Beta) la karibuni kisha utaunganisha kama kawaida na mara baada ya mawasiliano kati ya WhatsApp ya kwenye simu janja na kompyuta kuwepo unaweza ukaamua kuzima intaneti ya kwenye rununu na ukaendelea kupokea, kutuma jumbe bila kutegemea simu janja.
Iwapo utatumia WhatsApp Web toleo la Beta utakuwa na uhakika wa kufanya mawasiliano kama kawaida isipokuwa tu yale ya picha jongefu (video) na iwapo hutakuwa hewani kwenye WhatsApp ndani ya simu kwa siku 14 mfululizo basi akaunti yako itaondolewa na kukulazima kujiunga tena siku hiyo utakayojrejea kutumia WhatsApp Web toleo la Beta.
Mwisho, haimaanishi kuwa ukizima intaneti kwenye simu yako na kisha ukaendelea na mwasiliano ya WhatsApp kwenye kompyuta utakapokuja kuruhusu intaneti basi jumbe, picha, n.k hutavikuta la hasha! Kila kitu kitakuwepo na utaendelea kuwasiliana kama kawaida. Na kinyume chake ni hivyo hivyo.
Vyanzo: WaBetaInfo, mitandao mbalimbali
4 Comments