Facebook ni mtandao wa kijamii ambao una watumiaji wengi zaidi duniani lakini hivi karibuni kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka kumi na minane (18) takwimu zimeonyesha watu wanaoitumia wamepungua.
Kuna mengi ambayo Facebook imeyapitia katika miaka ya karibuni na hasa baada ya kukutwa na kashfa mbalimbali kitu kilichosababisha wenye mamlaka kutafuta mbinu za kuwabana wenye makampuni makubwa kwa lengo la kuwalinda wanaoitumia.
Kutokana na sheria mpya ndani ya Ulaya za kutaka makampuni ya teknolojia yanapokusanya data za watu ndani ya umoja huo, zichakatwe na kutunzwa kwenye kompyuta zenye uwezo wa hali ya juu zilizopo ndani ya umoja huo. Sasa kompyuta ambazo zinahifadhiwa data za Facebook na Instagram zinachakatwa kote Marekani na Ulaya.
Meta ndio inayoangalia hizo kompyuta zinazohifadhi data za Facebook na Instagram za Ulaya ambapo kwa jinsi mambo yalivyo hivi sasa wanafanya kinyume na ambavyo inatakiwa kuwa.
Kutokana na matakwa hayo mapya huenda Meta ikalazimika kusitisha huduma za Facebook na Instagram Ulaya kutokana na kwamba huenda ikashindwa kufanya kazi zake kama ambavyo inatakiwa kulingana na sheria mpya.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.