Zaidi ya gesi 100 zinazoweza kusababisha vifo hutolewa na betri zinazopatikana miongoni mwa mabilioni ya vifaa vinavyotumiwa na raia wengi duniani kama vile simu na laptop, utafiti wagundua.
Mabetri ya teknolojia ya Lithium-ion ni maarufu zaidi
Utafiti huo uliofanyika nchini China ulibaini gesi 100 zenye sumu kali zinatolewa na betri za aina ya Lithium-ion. Baadhi ya gesi hizo ni pamoja na kaboni monoksaidi (CO), ambayo inaweza kusababisha kujikuna katika ngozi, macho na pua mbali na kuathiri mazingira.
Watu wengi wanaotumia vifaa vya elektroniki vinavyotumia betri za teknolojia ya lithium-ion hawafahamu madhara ya kutotumia betri zenye ubora na pia betri kupata joto kupita kiasi (overheating), hasa hasa pale vinapochajiwa. Haya yamesemwa na watafiti hao kutoka taasisi ya ulinzi ya NBC nchini Czech pamoja na chuo kikuu cha Tsinghua nchini China.
Betri zilizopata chaji zaidi hutoa gesi zaidi za sumu ikilinganishwa na betri iliyo chini ya asilimia 50 ya chaji.
Utafiti huu unaonesha kuna umuhimu wa kuondoa simu yako kwenye chaji mara tu inapojaa, na pia si vizuri kulala na simu iliyojaa karibu yako. Tutaendelea kufuatilia kuona kama watafiti wengine watakubaliana na matokeo haya
Katika utafiti huo mpya, walichunguza aina ya betri za Lithium-ion. Mabetri haya ndiyo yamekuwa yakisifiwa sana kiusalama na yanatumika kwenye vifaa vingi zaidi vya elektroniki. Utafiti huu unaweza fungua milango ya uchunguzi zaidi unaoweza sababisha maboresho ya teknolojia nzima ya utengenezaji wake.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|