Kwa mwaka 2021 Huawei kutengeneza nusu ya idadi ya simu ukilinganisha na idadi ya simu walizotengeneza kwa mwaka 2020. Hii imechangiwa na vikwazo vya Marekani.
Katika taarifa ya Huawei kwa makampuni yanayosambaza vipuri kwake imesema kwa mwaka 2021 wanategemea kununua vipuri kwa ajili ya kutengeneza simu janja milioni 70-80, idadi hii ni chini kwa takribani asilimia 60 ukilinganisha na simu janja milioni 189 walizotengeneza na kuingiza sokoni mwaka 2020.
Vikwazo vya kibiashara vilivyowekwa na Marekani dhidi ya Huawei vimefanya hali iwe ngumu sana kwao kupata vipuri muhimu, hasa hasa vinavyohusisha mawasiliano ya 5G kwenye simu janja.
Ingawa wameweka lengo la simu janja milioni 70-80 bado kuna wanaoona wanaweza shindwa fikia idadi hiyo, kuna wengi wanaoona idadi kamili inaweza ikawa simu janja milioni 50 – hasa hasa ukichukulia ya kwamba wameshauza pia biashara nzima ya simu zinazobeba jina la Honor.
Tayari data za mauzo ya simu kwa mwaka 2020 zimeonesha kuporomoka sana kwa nafasi ya Huawei katika ushindani dhidi ya Samsung, Apple na Xiaomi.
No Comment! Be the first one.