Mwaka huu ukitaka kununua simu janja kutoka Samsung basi inaweza ikawa si jambo rahisi kusema kuchagua mara moja kwani zimetoka simu mbalimbali katika kipindi kifupi sana ikiwemo Samsung Galaxy A12.
Katika kupepesa macho yangu huku na kule nikakutana na simu hii ambayo ilitoka mwishoni mwa mwezi Disemba 2020. Kitu kizuri kuhusu simu hii ni kwa wale ambao tunapenda simu nzuri, bei ya kuhimilika basi Samsung Galaxy A12 inatufaa kwa sababu ya undani wa rununu yenyewe.
Sifa za Samsung Galaxy A12
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.5
- Ubora: LCD, 720x1600px
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: 3GB, 4GB na 6GB
Kamera :
- Kamera Kuu: Megapixel 48, 5, 2, na 2
- Kamera ya Mbele: Megapixel 8
Betri :
- Li-Ion 5000 mAh, uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W
Kipuri mama :
- Mediatek MT6765 Helio P35
Programu Endeshi
- OneUI 2.5, Android 10
Rangi/Bei :
- Bluu, Nyeusi, Nyeupe na Nyekundu
- Bei inaanzia $174 (zaidi ya Tsh. 400,200)
Kwa kuhitimisha tuu simu hii pia ina redio, teknolojia ya LTE lakini pia sehemu ya kuchomeka spika za masikioni bila kusahau teknolojia ya kutumia alama ya kidole.
Nini maoni yako kuhusu rurunu husika? Tupe maoni yako na usiache kutufuatilia kila inapoitwa leo kwa habari mpya zinazohusu teknolojia, sayansi kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360
One Comment