Simu ya Samsung Galaxy M02s imeanza kupatikana rasmi nchini India na inategemewa kuanza kupatikana katika mataifa mengine kote.
Simu hii ni simu yenye lengo la kukupatia kitu kizuri bila kuvunja akaunti yako ya benki.
Simu hiyo imeanza kupatikana nchini India kuanzia tarehe inategemewa kuanza kupatikana katika masoko mengine kama Afrika na bara la Ulaya kufikia mwezi wa Februari 2021.
Sifa na uwezo wa Samsung Galaxy S02s
Simu hii inakuja katika matoleo mawili
Toleo la RAM ya GB 3 na diski ujazo wa GB 32, na jingine ni la RAM ya GB 4 na diski ujazo wa GB 64.
- Programu endeshaji – Android 10
- Prosesa ya Qualcomm Snapdragon 450 na uwezo wa kusoma laini mbili za mawasiliano/simcard.
- Kwenye rangi kuna nyeusi, bluu na nyekundu.
- Simu zote zinakuja na uwezo wa kutumia memori kadi na zinasoma hadi microSD ya TB 1.
- Display – Inaukubwa wa inchi 6.5, kioo cha teknolojia ya Infinity V display (Full HD)
- Inakamera tatu nyuma. Kuna kamera kuu ya megapixel 13, pamoja na kamera zingine 2 za ziada za megapixel 2 (Macro sensor & Depth sensor).
- Kwa ajili ya selfi inakuja na kamera ya Megapixel 5
- Betri – Betri ni la kudumu muda mrefu, likiwa ni la mAh 5,000. Pia simu inakuja na teknolojia ya kuchaji kwa haraka ya kiwango cha 15W
Bei: Bei rasmi kwenye tovuti ya Samsung inaweka toleo la GB 32 nchini India kwa bei ya takribani Tsh 300,000/= wakati toleo la GB 64 likiwa kwa bei ya takribani Tsh 320,000/=. Tunafuatilia vyanzo vya Tanzania kufahamu bei zake zitakapoanza kupatikana Tanzania.
No Comment! Be the first one.