Hivi si ushawahi kufikiria kutumia namba yako moja ya WhatsApp katika simu mbili? Ukaichana na wewe kumbe hata kampuni ya WhatsApp imeliwaza pia jambo hili
Unakumbuka kuwa whatsApp mara ya mwisho ilitoa HII ili kuweza kutumia WhatsApp moja kwenye vifaa mbali mbali? hawakuishia hapo.
Hivi karibuni fununu kutoka WABetaInfo zinaeleza kuwa kipengele kinachojulikana kama ‘Companion Mode’ kitawezesha simu mbili kutumia namba moja ya WhatsApp.
Kingine ni kwamba kama vile unavyotumia WhatsApp Web ilikuabidi uscan kodi kwenye computer, basi ni hivyo hvyo itakubidi ku’scan kodi kwenye simu moja kupitia nyingine
Ukifanya hivyo ndio utaweza kutumia WhatsApp hiyo hiyo lakini kwenye simu janja nyingine.
Mpaka sasa japokuwa mpaka sasa hakuna ushahidi kamili juu ya siku ambayo mtandoa huu utaiachia rasmi hichi kipengele.
Kwa sasa unaweza kufurahia vipengele hivi vipya kutoka WhatsApp
Niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hii kutoka WhatsApp umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.