Zoezi la uandikishaji wa anwani za makazi linaendelea nchi nzima kwa lengo la kufanya maeneo yetu yaweze kutambulika kirahisi na hata kurahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali.
Kuna masuala mengi ambayo Tanzania inazidi kwenda mbele na kukubaliana na ukuaji wa teknolojia halikadhalika kwenda nayo sambamba. Hivi sasa si ajabu kusikia neno “Duka mtandao” ama kufanya malipo bila ya kwenda kupanga msururu kulipia huduma fualni. Haya yote hivi sasa yanaweza kufanyika popote pale na wakati wowote ule bila kujali ni saa za kazi au la!
Suala zima la amwani za makazi inaweza ikawa ni kitu kipya kwa wanachi wengi Tanzania lakini kwa nchi za wenzetu ikawa kawaida sana kutokana na kwamba zoezi hili lilishafanyika miaka mingi tuu huko nyuma lakini swali la kujiuliza “Anwani za makazi ni nini?”. Halikadhalika, postikadi ni nini?
Anwani za makazi ni mbinu ya kimsingi ya utambuzi wa kitu au maeneo mahali yalipo. Postikadi ni takwimu za kitaalamu za utambulisho kwenye anwani za makazi kumtambulisha mtu, kitu au mahali kwa usahihi zaidi.
Maana ya anwani za makazi na Postikadi katika kurahisisha utambuzi wa mtu, mahali/kitu.
Utambuzi wa postikadi kwa njia ya kidijitali
Teknolojia inakua kila leo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeweza kufanikisha watu kuweza kujua postikadi zao bila ya kutumia intaneti bali simu ya kiganjani kwa kupiga *152*00# na kisha chagua namba 3 halafu fuata maelekezo mengine hatua kwa hatua kuweza kufahamu postikadi ya kata unayoishi. Kama utakuwa umefuata maelekezo vizuri basi majibu yatakuwa “Ndugu mwananchi Postikodi (Postcode) ya kata ya Kibamba ni 16110“.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|
No Comment! Be the first one.