Zoezi la uandikishaji wa anwani za makazi linaendelea nchi nzima kwa lengo la kufanya maeneo yetu yaweze kutambulika kirahisi na hata kurahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali.
Kuna masuala mengi ambayo Tanzania inazidi kwenda mbele na kukubaliana na ukuaji wa teknolojia halikadhalika kwenda nayo sambamba. Hivi sasa si ajabu kusikia neno “Duka mtandao” ama kufanya malipo bila ya kwenda kupanga msururu kulipia huduma fualni. Haya yote hivi sasa yanaweza kufanyika popote pale na wakati wowote ule bila kujali ni saa za kazi au la!
Suala zima la amwani za makazi inaweza ikawa ni kitu kipya kwa wanachi wengi Tanzania lakini kwa nchi za wenzetu ikawa kawaida sana kutokana na kwamba zoezi hili lilishafanyika miaka mingi tuu huko nyuma lakini swali la kujiuliza “Anwani za makazi ni nini?”. Halikadhalika, postikadi ni nini?
Anwani za makazi ni mbinu ya kimsingi ya utambuzi wa kitu au maeneo mahali yalipo. Postikadi ni takwimu za kitaalamu za utambulisho kwenye anwani za makazi kumtambulisha mtu, kitu au mahali kwa usahihi zaidi.
Utambuzi wa postikadi kwa njia ya kidijitali
Teknolojia inakua kila leo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeweza kufanikisha watu kuweza kujua postikadi zao bila ya kutumia intaneti bali simu ya kiganjani kwa kupiga *152*00# na kisha chagua namba 3 halafu fuata maelekezo mengine hatua kwa hatua kuweza kufahamu postikadi ya kata unayoishi. Kama utakuwa umefuata maelekezo vizuri basi majibu yatakuwa “Ndugu mwananchi Postikodi (Postcode) ya kata ya Kibamba ni 16110“.
Hakuna tena kuhangaika kwani vitu vimesharahisishwa na kuletwa viganjani mwetu, kazi kwetu sasa kuweza kufahamu Postikadi za kwenye kata zetu.
Vyanzo: Mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.