Watumiaji wa sigara za elektroniki, yaani E-cigarettes, wanazitumia kwa sababu zinasifika ya kwamba ni salama zaidi dhidi ya magonjwa ya saratani (cancer) ukilinganisha na sigara za kawaida…ila inaonekana zinaweza kukudhuru kwa njia zingine pia.
Mwanaume mmoja Marekani anaweza kufanya maamuzi ya kutokutumia tena sigara za kielektroniki baada ya kuumia kutokana na mlipuko wa sigara ya hiyo (e-cigarette) iliyokuwa mfukoni mwake.
Tukio hilo lilitokea akiwa kazini na wenzake katika duka kubwa la uuzaji divai (Wine) jijini New York huko nchini Marekani.
Video za usalama za dukani humo zilifanikiwa kurekodi tukio zima la mlipuko huo. Video hizo zimeonesha Bwana Gooding, mwenye umri wa miaka 31 akipiga stori na wafanyakazi wenzake pamoja na mteja mmoja aliyekuwa anajiandaa kuondoka – ghafla mlipuko wa sigara hiyo ulisababisha watu kutawanyika kwa hofu huku wakimuacha Bwana Gooding akihangaika kuitoa sigara hiyo iliyokuwa ikiwaka na kulipuka kutoka mfukoni mwa suruali yake.
Tazama video hii inayoonesha jinsi jambo hilo lilivyotokea;
Mwanasheria wake amesema Bwana Gooding ameungua eneo kubwa la kwenye paja na kuna uwezekano akaitaji kufanyika upasuaji (surgery) kama sehemu ya matibabu.
Hadi sasa inaaminika mlipuko huo ulisababishwa na mfumo wa betri wa sigara hiyo.
Hii si mara ya kwanza kwa sigara za mfumo wa umeme kulipuka, na tayari wateja kadhaa wameshafungua kesi za madai dhidi ya makampuni kadhaa ya utengenezaji wa sigara hizi. Kwa kiasi kikubwa kuna uwezekano mkubwa Bwana Gooding naye akafungua mashitaka dhidi ya kampuni iliyotengeneza sigara iliyomlipukia.
Soma Pia – Sigara za Umeme, E-Cigarettes, zinasaidia watumiaji kuacha kuvuta sigara