iOS 14 ipo jikoni! Kwa wale wanaotumia bidhaa za Apple kama iPhone, iPad, n.k naamini watakuwa watakuwa wanafurahia iOS 13 huku wakiendelea kupakua maboresho pale yanapotoka. Nikuulize unafahamu ni lini toleo hilo litatoka?
Tunapotumia simu janja zetu tusipuuze hata kidogo suala la kupakua masasisho mbalimbali ambayo yanatolewa iwe kwenye Android au iOS kwani yanasaidia kuboresha kasoro ambazo zimeonekana kwenye programu endeshi husika na kuzidi kuifanya kuwa salama zaidi dhidi ya wadukuzi! Hatua hiyo itakufanya uepukane na gharama ambazo zinaweza kuzuilika.
Sasa kuna hili la iOS 14 ambalo linaelezwa kuwa litatoka kwenye majira ya joto (mwezi Juni) ambapo kimsingi linatazamiwa kuja kuondoa kasoro mbalimbali ambazo zipo kwenye iOS 13. Toleo hilo la kumi na nne linaonekana kuwa na muonekano wa kitofauti, kuweza kubadilisha akaunti ya Apple ID bila kuondoa iliyopo, kuweza kuhamisha huku na kule programu tumishi.
Toleo hilo kwa sasa lipo katika hatua ya majaribio kwa watu wachache sana (ndani kwa ndani) lakini mwezi Juni itakuwa imetoka kwa wale ambao wanaotumia iPhone, iPad. Tuambie kwa hayo machache ambayo yameshaanza kufahamika kidogo kidogo yanakuvutia? Tupe maoni yako.
Vyanzo: MacRumors, iMore