Samsung wana simu lukuki sokoni na wamekuwa wakitoa toleo moja baada ya jingine zikiwa zinapishana muda mfupi tuu na mapema mwaka huu walizindua Samsung Galaxy A52 ambayo inaonekana kuwa ni kivutio cha wengi.
Kama mdau wa masuala ya teknolojia simu hii imenivutia kwa namna yake hasa ukizingatia soko la ushindani lina rununu kedekede kiasi kwamba inakuwa vigumu kwa watu kuweza kuamua wanunue ipi kwa wakati ambao wanahitaji simu janja. Sifa za simu hii ni kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.5
- Ubora: Super AMOLED (1080*2400px, 90Hz); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB/256GB
- RAM: GB 4/6/8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 12, 5 na 5+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 32+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4500 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 25W (50% ndani ya dakika 30 tu)
Kipuri mama :
- Snapdragon 720G
Uzito :
- Gramu 189
Programu Endeshi
- UI 3.1, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi, Nyeupe, Zambarau na Bluu
- Gharama yake inaanzia $443 (zaidi ya Tsh. 1,018,900) bei ya ughaibuni
Samsung wameamua kutuletea vizuri. TeknoKona hatuna mengi zaidi ya kukuachia wewe uweze kufanya maamuzi ya kuipata au la!. Endelea kukaa nasi kwa habari mbalimbali za teknolojia kila siku.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment