Licha ya biashara zake za vifaa vya majumbani na simu janja bado kampuni ya Samsung inapanua wigo wake na kufanya biashara na makampuni mengine ya kuuza na kutengeneza simu.
Kwa Samsung hichi kitu kigeni kabisa kwani tangia mwanzo huwa wanuzaga vipuri vya simu kwa makampuni mengine ambayo kwa namna moja au nyingine wanaviweka katika matoleo ya simu zao…… mfano mzuri ni zile chipu ambazo walikua wanauziwa Apple.
Kwa UTG, itakua ni mara ya kwanza kwao kuuza maana teknolojia hii ya vioo walikua wanaitumia katika matoleo yao ya kukunja mfano samsung Galaxy Fold.
Mpaka sasa ijulikane kwamba Samsung ni msambazaji mmoja tuu wa vioo vya UTG, wazo la kuuza vioo hivi kwa makampuni mengine linakuja kuwa ni njia chanya ya kujitengenezea kipato.
Simu za kujikunja (Fold) kutoka Samsung Electronics zinasifika kuwa na utofauti mkubwa wa kioo ukilinganisha na zile ambazo zinatoka katika makampuni mengine kwa sababu ya teknolojia hii ya kioo.
Mteja ambae ni wa uhakika mpaka sasa hivi ambae wanae ni Google.Kwa haraka haraka habari hii inamaanisha kuwa kampuni ya Google iko mbioni kuja na simu ambayo itakua inajikunja (fold).
UTG ni kioo cha kwanza cha simu ambaco kianaweza kujikunja, kina uhalisia mkubwa na plastiki. Licha ya kampuni kuamua kuuza kwa wengine bado kuna maswali ya chini chini
Na maswali hayo mengi yakiwa yanataka kujua labda kampuni itatikisika na soko lake la simu za kujikunja kwani itakua tayari inaiuza kwa makampuni mengine.
No Comment! Be the first one.