Marekani yaweka vikwazo zaidi kwa Huawei. Katika hatua za mwisho zilizochukuliwa na Rais Trump dhidi ya Huawei ni kuwanyima uwezo wa kununua prosesa za Intel, hii ikiwa na vikwazo vingine kadhaa.
Serikali ya Bwana Trump inaondoka ikiwa imechukua hatua kadhaa zinazoumiza sana kampuni ya Huawei.
Kutokana na vikwazo vya Marekani ni muda sasa simu mpya za Huawei zinashindwa kuja na soko la Google PlayStore na apps nyingine maarufu za Google ambazo zimezoeleka na watumiaji wengi. Jambo hili limesababisha kuanza kushukwa kwa mauzo ya simu zake mpya.
Prosesa za Intel ni muhimu katika utengenezaji wa laptop na vifaa vingine vya kompyuta.
Hivi vikwazo zaidi kwa Huawei vitazidi kuendelea kuipa changamoto kubwa katika kutafuta njia ya kuendelea kukuza biashara zake.
Katika miaka michache kampuni ya Huawei imebadilika kutoka kuwa kampuni namba mbili katika biashara ya simu huku ikitishia kwa kasi kuing’oa Samsung kwenye nafasi ya kwanza hadi kuwa kampuni ambayo inahangaika kuendelea kushika nafasi ya pili – tayari kuna uwezekano mkubwa kwa mwaka hii ikapitwa na Xiaomi na ata Apple kama mambo yasipobadilika.
Katika taarifa iliyoonekana Ijumaa iliyopita kutoka umoja wa watengenezaji vipuri vya kompyuta nchini Marekani (Semiconductor Industry Association) katika hatua za mwisho za Serikali ya Rais Trump zilizochukuliwa zimewakata kuendelea kuudha bidhaa na teknolojia kadhaa kwenda kwa Huawei ambazo hazikuwepo katika katazo la mwanzo.
Katazo hili jipya linahusisha pia prosesa za Intel na ata baadhi ya bidhaa zinazohusisha teknolojia za uhifadhi data (flash storage).
Kwa ujumla wake biashara zenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 280 kati ya Huawei na makampuni ya kiteknolojia ya Marekani ipo kwenye vikwazo kwa sasa.
Huawei na wafanyabiashara wengi wanaangalia kama serikali mpya ya Rais Biden itafanya mabadiliko ya kisera dhidi ya China na Huawei.
No Comment! Be the first one.