Nokia G11 ni simu janja iliyozinduliwa lakini haikuwa na shamrashamra za matangazo kuhusiana na uzinduzi wake na badala yake watu walishangaa kuikuta kwenye tovuti ya Nokia kama bidhaa yao mpya.
Simu hii inafanana kwa karibu kabisa na Nokia G21 katika maeneo mengi tuu lakini utofauti wake unaonekana zaidi kwenye kamera kuu na ni nyepesi zaidi. Simu hii ina sifa hizi:
Kipuri mama|Muonekano
HMD Global wameamua kutumia kipuri mama sawa na kile walichoweka kwenye Nokia G21 hivyo basi, rununu hii pia imewekwa Helio G35. Kwa upande wa muonekano simu janja hii ina kioo chenye urefu wa inchi 6.5 cha LCD na kina ubora wa 90Hz.
Memori|Kamera
Tofauti kubwa kati ya Nokia G11 na G21 inaonekana hapa kwani toleo la Nokia G11 kamera kuu ina MP 13 na nyingine mbili ambzo zote zina MP 2. Kamera ya mbele ina MP 8. Upande wa memori ni GB 3 za RAM na 32GB za diski uhifadhi halikadhalika, inawezekana kuweka memori ya ziada ya mpaka GB 512.
Uwezo wa betri|Mengineyo
Kivutio kikubwa cha kwenye simu hii ni uwezo wake wa betri; ina betri yenye 5050mAh, inatumia teknolojia ya kuchaji haraka ya 18W, inatumia USB Power Delivery 3.0, inakuja na toleo la Android 11 lakini kuweza kuhamia kwenye Android 12 baada ya muda mfupi.
Simu hii inauzwa kwa zaidi ya Tsh. 414,000 (bei ya ughaibuni) na itapokea masasisho ya programu endeshi kwa miaka miiwli (Android 12 na Android 13) na miaka mitatu ya maboresho kuifanya simu kuwa salama kila mwezi.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.