Mitandao mbalimbali hivi sasa ipo na habari zinazoihusu Tecno na familia kuzidi kuongezeka kwani Tecno Camon 18T ipo mbele ya macho ya watu kwa malengo ya kwamba ipate soko kirahisi.
Mwaka 2021 upo ukingoni kumalizika na makampuni mengi duniani ambayo yanafanya biashara ya kutengeneza simu janja yanafanya hima kumaliza mwaka na toleo jipya la rununu. Tecno ni moja ya makampuni hayo ambayo safari hii wanasifika mwafamilia mpya katika ule mwendelezo wa simu janja za Tecno Camon.
Tecno Camon 18T toleo mojawapo kutoka kwenye familia ya Tecno Camon ambayo makala hii inalenga kuziongelea zile sifa ambazo wateja wa simu janja tunataka kuzifahamu kabla ya kununua rununu. Sifa hizo ni:
Muonekano | Prosesa
Ingizo hili jipya la 18T lina kioo chenye urefu wa inchi 6.8 ambacho kina ungávu wa ya juu halikadhalikamuundo wa kamera ya mbele ipo ndani ya kioo ambayo inagawa kioo nusu kwa nusu. Kipuri mama kilichopo kwemye Tecno Camom 18T ni MediaTek Helio G85.
Kamera | Uwezo wa betri
SImu hii ina kamera tatu nyuma, taa mbili za kuongeza mwanga lakini vilevile kuna kamera moja mbele ambayo pia ina taa mbili za kuongeza nakshi kwenye picha/video. Kamera zake zina MP 48 na mbili MP 2 kila moja. Kamera ya mbele ina MP 48. Betri la kwenye simu lina mAh 5000, 18W za teknolojia ya kuchaji haraka.
Memori | Sifa nyinginezo
Hapa tunakutana na chaguo moja la kwenye memori kwa maana ya RAM ni GB 4 na diski uhifadhi ni 128GB. Kamera zote za nyuma na mbele zina uwezo wa kurekodi picha za mnato katika ubor wa 1080px. Ina redio, sehemu ya kuchomeka spika za masikioni, inatumia Android 11, inapatikana katika rangi Nyeupe, Kahawia na Zambarau.
Tayari imeshaingia sokoni na bei yake ni karibu $169 ambazo ni sawa na zaidi ya Tsh. 389,000 iwapo utainunuliwa ughaibuni. Je, kwa sifa za simu hii unaona itauzika kwa kiwango cha juu?
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360 na mitandao mingine
No Comment! Be the first one.