iMessage ni huduma ya kutuma na kupokea ujmbe (inajumuisha maandishi, video na picha) katika vifaa vya iOS tu. Huduma hii imekua maarufu sana na inawafanya hata watumiaji wengi wa vifaa vya iOS kutohama na kwenda katika vifaa vingine kama vile vya Android.
Hapo awali kulikua na fununu nyingi sana ziliingia kwamba pengine labda Apple wangepeleka huduma yao hiyo kayika programu endeshaji ya Android. Hiyo ni sawa ingewaongezea watumiaji wengi sana wa huduma hiyo.
Lakini Apple wanasema kwamba wakiamua hivyo hilo litawaumiza sana kuliko kuwasaidia. Hii ni kwa mantiki kwamba sawa wataongeza watumiaji (Android) lakini watu wengine wanaweza wakahama kutoka kutumia iPhone na kuhamia simu zingine kama vile Samsung.
Kama huduma itapaikana kila sehemu basi soko la simu za iPhone litashuka wakati huo huo iMessage itakuza watumiaji wake na jambo hili litawaumiza sana Apple kuliko kuwasaidia.
Apple walikata kuanzisha iMessage kwa ajili ya Android tangu mwaka 2013. kumbuka huduma kama iMessage na Facetime ndio zinawafanya watumiaji wa iPhone, iPad, na Mac wazidi kubaki na kutumia vifaa hivi (labda wana sababu zingine) pengine wangeshalihama kama zingepatikana kwingine.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Sanduku La Maoni, Pia Tembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Vyanzo: HTech, MacRumors
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Hashiman (@hashdough) Nuh
Mhariri Wa TeknoKona Na Mmoja Kati Ya Wafuasi Wa Teknolojia! Naomba Tuikuze TeknoKona Wote Basi. Ningependa Kusikia Kutoka Kwako Nitumie Barua Pepe hash@teknokona.com
No Comment! Be the first one.