Unafahamu kuwa Facebook, WhatsApp na Intagram zilikumbwa na tatizo la muda lililosababisha mawasiliano kuwa magumu? Wengi walipata changamoto duniani kote.
Katika mawasiliano ya wengi kwa miaka mingi tuu sasa yanafanyika kwa wingi zaidi kupitia WhatsApp halikadfhalika Instagram na Facebook ambazo zimekuwa na mchango wa kipekee katika kufanya watu wawasiliane kwa wepwsi kabisa. Sasa hakika wale ambao kwa namna moja au nyingine tulikuwa tukiperuzi kwenye WhatsApp, Facebook na Instagram mishale ya saa 7 usiku siku ya Alhamisi basi tulipata changamoto kwani mitandao hiyo ya kijamii ilikuwa na shida.
Ripoti zinaonyesha tovuti ya Facebook ilikuwa na matatizo zaidi ya 112,000 yaliyoripotiwa, 101,000 ya watumiaji wa Instagram na 516 ya watu kwenye WhatsApp walieleza changamoto walizokumbana nazo nyakati za saa 7 usiku wa Alhamisi.
Hii imekuwa ni mara ya pili kwa tatizo hili kujitokeza katika kipindi cha karibu mwezi mmoja; katikati ya mwezi Machi changamoto hiyo ilijitokeza kwenye Facebook, WhatsApp na Instagram na kudumu kwa karibu saa nzima. Facebook walikuwa kimya tuu lakini inaaminika wahusika walikuwa kwenye zoezi za kuhifadhi taarifa za watumiaji wake ndio maana zoezi hilo likaleta malalamiko kutoka sehemu nyingi duniani.
Tuambie ewe msomaji wetu je, na wewe ulikuwa mhanga wa kutoweza kutumia Facebook, WhatsApp na Instagram siku ya Alhamisi mishale ya saa 7 usiku?
Vyanzo: Gadgets 360, Forbes
No Comment! Be the first one.