Tukiangazia simu janja ambazo Samsung wametoa mpaka sasa kwa mwaka huu tu inaweza ikawa vigumu kuweza kupata uchambuzi wake kila moja kwani ni nyingi na si hilo tuu kwani kuna hii Samsung Galaxy A03s ambayo imeshaletwa mbele ya macho yetu.
Kwenye ulingo wa simu janja Samsung wameendelea kuwaangalia wateja mbalimbali kwa maana ya kwamba wale wenye uwezo wa kununua simu janja na hata wale ambao wanaweza kuwa na rununu zilizo katika daraja la kati. Samsung Galaxy A03s ni mojawapo ya rununu ambazo zipo kwenye “Daraja la kati”. Fuatana nami kuweza kufahamu sifa za aimu janja husika.
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.5
- Ubora: IPS LCD (720*1600px); ung’avu wa hali ya juu+kamera ya mbele imeingia kwa ndani kidogo mithili ya bonde la ufa (umbo la herufi V)
Memori :
- Diski uhifadhi: 32GB/64GB+sehemu ya kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 3/4
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 13 na mbili zina MP 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 5
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W
Kipuri mama :
- MediaTek Helio P35
Uzito :
- Gramu 196
Programu Endeshi
- One UI 3.1, Android 11
Rangi :
Nyeupe, Nyeusi, Bluu
Bei ya simu hii inaanzia $150|zaidi ya Tsh. 345,000 huko ughaibuni na tayari imeshaingia sokoni. Kumbuka kufuatilia TeknoKona kila siku pia unaweza KUBOFYA HAPA kuweza kusoma makala mbalimbali zinazohusu simu.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.