Alix Tichelman (28) ni mwanadada maarufu kwa kazi ya kujiuza ambaye amepata adhabu ya kwenda jela miaka sita baada ya kukubali kuwa aliua bila kukusudia. Hili sio jambo geni kwa baadhi ya watu kuona kuwa watoaji huduma hao wakijuhusisha pia na madawa ya kulevya
Kesi hii kubwa wakati ikiendelea watu walishangazwa kuona Alix Tichelman kukubali mashtaka kwamba Aliua bila kukusudia na kuhusika na madawa ya kulevya.
Bw. Forrest Hayes, kutokana na mafanikio yake amekua mmoja kati ya wamiliki wa magari na maboti ya kifahari. Kifo chake kilitokea kwenye moja kati ya boti zake. boti lakw alilipa jina la ‘Escape’ ikiwa na maana ya kutoroka (kimbilio)
Alifariki dunia Novemba mwaka 2013 baada ya kupewa madawa ya kulevya ambayo yalimzidi nguvu na usiku wa kustarehe na Alix Tichelman (Malaya wa kulipwa) katika boti yake. Kamera iliyopo kwenye boti ilinasa uwepo wa Alix katika boti hilo siku ya tukio.
Polisi walisema kuwa Bw. Hayes alimpata Alix katika mtandao wa SeekingArraignment.com na baada ya hapo wakawa wanakutana mara kwa mara kwa lengo la kufanya mapenzi na kujipatia madawa. Polisi pia walisema kuwa wateja huwa wanamlipa Tichelman zaidi ya dola za kimarekani 1000
Tichelman alikubali makosa hayo kwa kuwa mahakama ilikua na ushahidi wa kutosha. Kamera ya kiusalama iliyotegeshwa imeonyesha Alix akikusanya virago vyake, kuruka mwili wa marehemu hayes (51) na kumalizia glasi yake ya mvinyo kisha akafuta ‘counter’ na kujificha uso wake kidogo kisha akaondoka katika boti hiyo Novemba 23
No Comment! Be the first one.