Motorola wapo njiani kuja na simu janja mpya ambayo inaonekana kuna nguvu nyingi zimewekezwa kuhakikisha kuwa kamera ya rununu husika inakuwa ni yenye ubora wa kuvutia.
Zimekuwepo taarifa mbalimbali zikihusisha Motorola kueta simu janja ijayo mbele ya macho ya watu ambayo inayo kamera ya ubora wa hali ya juu ambapo awali iliaminika kuwa simu hiyo ina kamera yenye 200MP iliyotengenezwa na Samsung lakini mambo ni tofauti kwa kile ambacho kimeonekana. Sifa za kamera nyingine mbili za nyuma zinaamika kuwa na MP 50 na nyingine 12MP na kufanya simu hii kuwa na jumla ya kamera tatu kwa nyuma pekee.
Mengineyo
Simu hii ijayo kutoka Motorola itakuwa na kioo chenye urefu wa inchi 6.7 aina ya OLED na kuwa na kipuri mama cha Snapdragon 8 Gen 1 Plus. Uwezo wa betri lake unategemwwa kuwa na 4500mAh, 125W za teknolojia ya kuchaji haraka kwa kutumia waya, 50W iwapo utachaji haraka bila kutumia kiunganishi.
Kuna uwezekano wa simu hii kuzinduliwa mwezi Julai mwaka huu na bado tuna miezi kadhaa hivyo ni wazi kwamba fununu hizi zitaendelea kutoka. Nikusihi tuu kuendelea kutembelea tovuti yetu kila machweo na mawio kuweza kuhabarika.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.