Mwezi Julai mwaka huu ulikuwa na ingizo jipya la simu janja kutoka Motorola ambao wameendelea kuja na rununu ambazo zinaendana na kile ambacho wateja wanahitaji sokoni. Motorola Edge 20 ilikuwa ni moja ya simu janja ambayo ilikuwa na habari lukuki za chini kwa chini.
Makampuni mengi siku hizi yanaweka ubunifu, nguvu nyingi kwenye vitu ambavyo vitaiuza rununu kwa haraka mara tu pale itakapoonekana. Motorola Edge 20 ni moja ya simu hizo ambapo imewekwa nguvu nyingi kuanzia kwenye ubunifu wa muundo wake mpaka kwenye kamera. Fuatana nami kuweza kufahamu undani wake:
Kamera|Muonekano
Kwa muonekano ni simu janja nyembamba isiyochukua nafasi kubwa na si nzito. Kwenye kamera ile kuu ina MP 108, inayofuatia ni MP 8 ambayo unaweza kukuza kitu mara 3 zaidi na ya mwisho imewekwa MP 16 bila kusahau taa 2 za kuongeza mwanga sehemu hafifu.
Kioo|Memori
HIi simu ina kioo chenye urefu wa inchi 6.7 cha ubora wake ni OLED pamoja na kamera ya mbele iliyowekwa chini ya kioo lakini katika mtindo wa kufanya mbele kuwepo kwa shimo dogo na ina MP 32. Upande wa memori simu hii ina GB 8 za RAM, 128 GB au 256 GB-diski uhifadhi.
Betri|Mengineyo
Betri lake lina 4000mAh, 30W za teknolojia ya kuchaji haraka, inatumia USB-C 2.0. Ni simu janja yenye teknolojia ya 5G, kipuri mama ni Qualcomm Snapdragon 778G 5G, teknolojia ya kutumia alama ya kidole imewekwa kwenye kitufe cha kuzima/kuwasha simu, inatumia Android 11 lakini ipo kwenye mpango wa kuweza kuhamia hadi Android 13.
Gharama yake inaanzia $593.99|zaidi ya Tsh. 1,366,177 kwa bei ya ughaibuni na tayari imeshaingia sokoni rangi zake ni Kahawia, Nyeupe, Bluu.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment