Facebook ambayo kwa kiasi fulani imepoteza uaminifu kwa wateja wake kutokana na mabo mbalimbali yaliyoikumba kampuni hiyo mwaka huu sasa wamebuni njia ya kuwavutia watu.
Kundi kubwa ambalo linatumia Facebook ni vijana na katika kujaribu kuwarudisha watu wahusika wametoa programu tumishi, TikTok (Lasso) ambayo kazi yake ni kuweza kusambaza picha jongefu fupifupi.
Programu hiyo inalenga vijana wanaochipukia ambao kwa ndio kundi kubwa linalotumia mitandao ya kijamii. Kimsingi Lasso inakupa uwanja mpana wa kuweza kuwashikisha wengine picha za mnato kutoka kwenye simu yako au za kutengeneza muda huohuo.
Lasso-Programu tumishi mpya mahususi kwa ajili ya kusambaza picha jongefu zisizozidi urefu wa sekunde 15.
TikTok inapatikana kwenye Android/iOS ukiwa na uwezo wa kujiunga kupitia jina/barua pepe pamoja na nywila unayotumia kuingia kwenye akaunti ya Facebook/Instagram au ukajiunga upya tu mara baada ya kupakua Lasso.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|