Mtandao wa kijamii wa facebook umekuja na mpangilio mpya katika makundi (Groups) lengo likiwa ni kufanya mazungumzo yawe rahisi Zaidi.
Hapa wenye mamlaka makubwa (yaani ma admin) na watumiaji wa kawaida wa makundi haya watakua na uwezo wa kutumia huduma hii mpya
Vipengele vyote vipya vimekusanywa katika eneo moja, na uzuri ni kwamba unaweza kuingia na kutoka katika makundi yako kwa haraka Zaidi ukitumia huduma hii
Kinachofanyika ni kwamba makundi yote –ambayo unahusika nayo — yatakua yamejikusanya hapa (eneo moja)
Katika eneo hilo utaweza kuona mambo mbali mbali bila kusahau yale mambo ambayo unakua umepitwa nayo kwa muda
Kingine ni kwamba unaweza uka’pin makundi yako pendwa kwa juu pale ili kuweza kuyafikia kwa urahisi Zaidi
Ukiingia katika kundi lolote katika mtandao wa Facebook basi utakutana na menu nyingine ambayo ina vipengele kama vile ‘shops’ na hata ‘events’
Kingine ni kwamba mtandao huo umeweka kipengele kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Facebook channels’ ukiwa ndani ya kundi (Group)
Huduma ya Channels kazi yake kubwa ni kwamba inasaidia watu katika kuongelea na kuchangia mada moja
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, hii umeipokeaje? Je wewe ni mtumiaji wa makundi katika mtandao hu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.