Cable News Network (CNN) imesema mpaka kufikia mwaka 2022 itakua imeshaanzisha huduma mpya ambayo itajulikana kama CNN Plus nahuduma hii itakua ni ya ku’stream
Ni wazi kuwa siku hizi huduma za Ku’stream zimekua ni nyingi sana na hivyo pengine labda mtandao wa habari wa CNN umeona unabaki nyuma nyuma sana.
CNN mpaka sasa hawajaweka wazi kwamba huduma hiyo itakua inapatikana kwa gharama gani lakini wamegusia kidogo kwamba inaweza ikahusisha vipindi vya zamani vilivyokuwa na majina makubwa makubwa.
Baada ya kuanzishwa kwake ndani ya miezi sita mpaka tisa ina mpango wa kuajiri wafanyakazi 450. Ukiachana na hayo vile vile huduma itahusisha vipindi vile vya ‘live’ na vile vinavyopendekezwa sana na watazamaji n.k.
CNN wamesema kwamba wakati CNN plus inatambulishwa, huduma hiyo kwa mwanzo haitahusisha matangazo lakini hawakuweka wazi kuwa mbeleni itakuawaje.
Kingine katika uzinduzi usitegemee kuwa CNN Plus itakua inajitegemea na App yake, la hashaaa… App ile ile ya CNN itakuwa inatumika na wale ambao wanataka kuingia katika CNN Plus, ila lazima kuwe na taratibu za kufanya hivyo.
Japokuwa kwa haraharaka unaweza sema CNN Plus mbona ina kila namna ya kufanana na CNN kwa kila kitu, lakini wenyewe wanasema kuwa kutakuwa na tofauti kedekede.
No Comment! Be the first one.