Kwa sasa kuna huduma mpya ya Google inaitwa Google Chat, Google Hangouts itafungwa lakini kabla ya hapo itahamishiwa kwenye huduma ya Google chat.
Mara ya kwanza kabisa huduma ya Hangouts ilikua inapatikana katika mtandao wa kijamii wa Google Pus ambao nao baada ya muda tuu ulifungwa—pengine labda Google inafunga sana baadhi ya bidhaa zake eeh?
Kazi kubwa ya hangouts katika mtandao huo ilikua ni kutuma meseji kwa marafiki au hata kupiga zile simu za video.
Mwanzoni mwa mwaka huu ndio tumeshuhudia huduma ya chat kutoka Google kuunganishwa katika huduma kadha wa kadha kutoka Google.
Novemba 2022 ndio mwisho wa kutumia Hangouts maana itakua imeshafungiwa kabisa, na kama ulikua unatumia huduma hiyo sana sana nna wasiwasi mpaka sasa utakua ushaambiwa kuhamia katika chat.
Kama ulikua unatumia Hangouts ndani ya mtandao wa Gmail basi itakua inakupeleka moja kwa moja katika chat ukiwa unataka huduma hiyo.
Hapa kikubwa ni kwamba hakuna kikubwa kilichobadilika sana maana chat ina mfanano wa kiamtumizi na hangout na hata mitandao mingine kama slack.
Mitandao hii huwa inawezesha utumaji wa jumbe kwa makundi na hata zile za siri (kwa umoja) na kadhalika
CHANZO: The Verge
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, hii umeipokeaje? Je utakuwa tayari kuanza kutumia huduma hii?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.