Hivi sasa ulimwenguni habari ni kuhusu COVID-19 ambavyo vinasababisha homa ya mapafu na kuweza kusababisha kifo. Dunia ya leo ipo “Kiganjani” hivyo watu wana uwezo wa kupata taarifa mbalimbali wakiwa popote na muda wowote kupitia WhatsApp.
Watu wengi sana wameshapoteza maisha yao kutokana na homa kali ya mapafu inayosababisha na virusi vya Corona aina ya COVID-19. Sasa njia mbalimbali zinatumika kukabiliana na janga hilo lililoikumba dunia bila kusahau elimu kwa umma ili kuweza kuutokomeza hatimae hali irudi kuwa kawaida kwa kuondokana na tatizo hili.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa namba maalum ambayo watu wanaweza kuwasiliana nao kupitia WhatsApp wakati wowote ili kuweza kupata elimu, taarifa mbalimbali kuhusu virusi vya Corona. BOFYA HAPA kuweza kuanzisha mazungumzo ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu virusi vya Corona.

Kupitia hapo watu wataweza kupata mengi kutoka shirika lenye dhamana ya kushughulikia afya duniani. Kwa hatua hii ina maana watu wanaweza kupata vitu vingi na vya uhakika kutoka kwenye chanzo cha kuaminika lakini pia tusipuuze taarifa zinazotolewa na WIZARA YA AFYA kuhusu virusi hivyo.
Vyanzo: GSMArena, WHO
2 Comments
Comments are closed.