Kwa wale amabao wanapenda simu janja za iPhone ambazo ni ndogo na zinakaa vizuri katika mikono yao matoleo haya (kama iPhone 12 Mini) yalikua ndio kimbilio lao.
Unaweza ukajiuliza ni kwanini hili limetokea mpaka kampuni iwe na uamuzi wa kutoendelea na uzalishaji wa simu hii, lakini kikubwa ni kwamba mauzo ya toleo la aina hii ya simu yamekua ni madogo sana.
Ukiachana na hilo ni kwamba bado kampuni inakuja na toleo la iphone 13 ndogo ambayo inaweza ikajulikana kama iPhone 13 Mini ndani ya mwaka huu.
Vyanzo mbali mbali vimesema kuwa pengine toleo hilo halikuafanya vizuri sokoni kwani Apple walitoa toleo la pili ya iPhone SE (ambayo nayo ni ndogo) miezi sita baada ya kutoa tolea la iPhone 12 Mini.
Inakuwa ni vigumu kwa yeyote ambae anapenda iPhone ndogo kuhama kutoka iPhone SE (toleo la pili) na kwenda kununua iPhone 12 mini ndani ya kipindi cha miezi sita tuu.
Aidha vyanzo mbalimbali bado vinadai kwamba Apple wataacha kabisa kutengeneza simu zenye vioo vidogo vya inchi 5.4 ifikapo mwaka 2022.
No Comment! Be the first one.