Fikiria kama utaweza kuwa na uwezo wa kuingia katika mitandao mikubwa (yakijamii) na kutumia vifaa vya kielektroniki kwa ku’Log In’ bila hata ya kutumia neno siri.
Makampuni makubwa na nguli katika swala zima la teknolojia (Apple, Google, Microsoft) wamedhamiria kuwezesha swala hili na wako katika hatua za mwanzo.
Kumbuka kama hili litawezekana ni lazima kwanza liwezeshwe katika mitandao na vifaa ambavy viko chini ya himaya yao mfano iPhone, gmail, facebook n.k
vile vile hapa inakubidi ufikirie zaidi hata katika swala zima la progarmu endeshaji kama vile iOS, Android na vivinjari (Browser) kama vile Edge na Chrome pia vitaweza kuwa na huduma hiyo.
Lingine ambalo limegusiwa ni kwamba licha ya kwamba njia hii kuonekana kama vile haina uimara zaidi wa kiusalama katika jicho la haraka haraka….
Makampuni hayo yanafanya kazi ili kuhakikisha kuwa taarifa za ulinzi na usalama zinachukuliwa kama ni nyeti sana na zinahifandhiwa vizuri.
Kwa haraka haraka ni kwamba Ku’Log In’ bila kutumia Nywila (password) kunawezekana sana na habari zilizopo ni kwamba simu ya mtumiaji ndio itakua kama daraja (nywili) ili kuingia katika mitandao fulani au App.
Yaani hapa ni kama vile unavyofungua simu yako kwa kutumia alama za michoro (pattern), alama za vidole (fingerprint) au kwa kutumia PIN, hiyo inabidi iwe inatosha kuwa namna ya kulog in katika mitandaa na App kadha wa kadha.
Makampuni hayo matatu (Apple, Microsoft Na Google) yanadai kuwa teknolojia hii itegemewe mwakani. Japokuwa bado haijawekwa wazi kwamba ni njia gani au mbinu gani zitatumika katika kuliwezesha hilo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, hii umeipokeaje? je huduma hii ikianza kutumika uko radhi kuachana na njia ya kawaida na kuanza kutumia hii?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.