Kwa Snapchat sio kitu cha kushangaza sana kuja na teknolojia kama hizi si unakuambuka ile miwani inayojulikana kama Spectacles?
Sasa hivi inakuja na Drone ambayo itakua mahususi kwa ajili ya kupiga selfie za hapa na pale pia na video ambazo moja kwa moja zitaweza kusambazwa katika mtandao huo wa kijamii.
Drone hii imepewa jina la Pixy, na kwa sasa Drone hizi zinapatika kwa kaisi kikubwa ufaransa na marekani kwa huko sheria za kurusha drone hazina mkazo sana kama mataifa mengine.
Meet Pixy. Your friendly flying camera. Pixy brings magic to every moment, all you have to do is let it fly! #FlyWithMe pic.twitter.com/GAh8znI76I
— Pixy (@snappixy) April 28, 2022
Kwa taarifa kutoka Snapchat ni kwamba wameona mitandao mingine mingi ya kijamii ikijiwezesha zaidi na kuunda teknolojia zingine nyingi ambazo zinatumika sambamba na mitandao yao ya kijamii
Hii ni moja kati ya njia ambayo imewasukuma kuja na teknolojia hii ukiachana na sababu kuwa wanataka kuwaletea kilochobora kabisa watumiaji wa mtandao wao.
Kumbuka ili kurusha Drone bado inabidi uwe na kibali, ukiachana na hayo vyanzo mbali mbali vimekua na wasiwasi kuhusiana na udogo wa drone hii.
Wengi wanajiuliza je itakua na mitambo imara ambayo imejidhatiti katika kufannya kazi yake kama Drone nyingine? nafikia jibu haliwezi kupatikana mpaka wajaribu sio?
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Nipe Mtazamo Wako Hasa Katika Mazingira Yetu Ya Tanzania, Unafikiri Watu Wanaweza Kufanikisha Katika Kutumia Teknolojia Hii Kwa Urahisi Kabisa?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.