Miaka miwili baadae tangu Samsung Galaxy A30s itoke sasa Android 11 imegonga hodi kwenye rununu husika ikikiwa ni muendelezo wa simu janja mbalimbali kuwa na uwezo wa kutoka kwenye toleo moja hadi jingine.
Mwaka 2019, Samsung Galaxy A30s ikiwa na Android 9 ambapo kwa wakati ule ndio ilikuwa habari ya wengi kwenye simu janja zinazotumia rogramu tumishi husika. Mwaka hadi mwaka toleo la Android likawa linatokka na sasa tupo kwenye Android 11.
Kwa watumiaji wa Galaxy A30s hii ni habari njema kwao kwani sasa wanaweza kupakua Android 11 baada ya kuwa wavumilivu wakisubiri toleo hilo la programu endeshi husika pamoja na ile sura ya mbele (UI 3.1).
Angalizo/Muhimu kufahamu
Suala la kupakua programu endeshi si kitu kigumu kabisa iwapo utazingatia mambo muhimu kabla ya kuanza zoezi zima. Kwanza kabisa ni lazima kuhakikisha simu janja ina chaji kuazia 50% na kuendelea, ina nafasi/memori angalau GB 1.5 au zaidi. Kitu cha muhimu na pengine uti wa mgongo wa kufanikisha suala zima hakikisha una kifurushi cha intaneti angalau GB 1.3 na kuendelea.
Leo imekuwa ni zamu ya rununu hii je, kesho itakuwa ni simu gani? Jibu ya hilo swali ni kuendelea kutufuatilia kila siku ili kuweza kuhabarika.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.