Kuja kwa uwezo wa kuhama mtandao wa simu bila kubadili namba ya simu umekuja na changamoto ya jinsi ya kurahisisha huduma za pesa za simu bila kujali mtandao wa simu ambao mtu anatumia. Airtel, Tigo na Zantel wamerahisisha hili kwa sasa.
Airtel, Tigo na Zantel kupitia huduma zao za Airtel Money, Tigo Pesa na EzyPesa wamefanya zoezi la kutuma na kupokea pesa kwenye huduma zao kuwa rafiki zaidi kwa watumiaji wao. Kuanzia sasa mtumaji pesa kutoka kwenye mitandao hiyo kwenda huduma nyingine katika mitandao hiyo atakatwa gharama ya kutuma ile ile kama anayokatwa akiwa anamtumia mteja wa mtandao kama wake.
Yaani kama mtu anatuma pesa kutoka Airtel Money kwenda Tigo Pesa basi atakatwa gharama za kutuma kama zile ambazo huwa anakatwa akituma kwenda huduma ya Airtel Money.
Jamhuri, Dodoma: Je wajua kuwa ukituma pesa kwenda mtandao mwengine makato ni yaleyale ya kutuma kwenda mtandao wako? #TaifaMoja #BilaMipaka pic.twitter.com/vJ9Op19ApT
— Taifa Moja (@TaifaMoja) March 5, 2017
Kwa kiasi kikubwa uamuzi huu utawasaidia sana wateja wao hasa hasa kwa wakati huu ambao mteja wa mtandao wowote anaweza kuhama mtandao wa simu kwa urahisi zaidi. Jambo hili linafanya uamuzi wa kuhama uwe rahisi kwa watu ambao huwa wanategemea sana huduma za kutuma na kupokea pesa.
Airtel, Tigo na Zantel wamejiunga katika kusambaza elimu kwa wateja juu ya huduma hii kupitia kampeni ya Taifa Moja ambayo tayari inafanyika katika mikoa mbalimbali. Kampeni hiyo imedhaminiwa na taasisi tanzu ya Benki ya Dunia, IFC.
Vipi je wewe ni mteja kati ya huduma hizi? Una maoni gani juu ya hili?
One Comment
Comments are closed.