Kampuni ya Apple imeweka zawadi ya dola milioni 1 kwa mtu atakayeweza kudukua iPhone na kuwapa taarifa ya jinsi walivyofanikiwa kufanya hivyo.
Pesa hiyo ambayo ni zaidi ya Tsh Bilioni 2 zinalenga kuhakikisha wadukuaji hawauzi teknolojia hizo kwa makampuni mengine. Ingawa kwa muda mrefu Apple wamekuwa wakiichukulia sifa ya kuwa iPhone haziwezi kudukuliwa hali imekuwa tofauti hivi karibuni. Kuna makampuni ya kiusalama hasa ya Israel yaliyoonesha tayari kuwa na uwezo huo.
Kwa dau hili wanategemea mtafiti mdukuzi akifanikiwa kuona tatizo au njia ya kudukua iOS au MacOS achukue uamuzi wa kuwapa taarifa hizo Apple na si yeye kutumia taarifa hizo kwa manufaa yake mwenyewe au kuuzia makampuni mengine.
Dau hili la dola milioni 1 za Kimarekani kwa mtu atakayeweza kudukua iPhone au MacBook ni kubwa sana kwani kipindi cha nyuma wamekuwa wakitoa zawadi ya dola laki 2. Uamuzi huu unaonesha kuwafanya wadukuzi kuvutiwa zaidi na kuwapa Apple siri ya mafanikio yao badala ya wao kuyauzia makampuni ya kiusalama kama vile …. kutoka Israel.
Hivi karibuni imeonekana mashirika ya kiusalama kama vile FBI yapo tayari kulipia huduma hizo pale ambapo msimamo wa Apple umekuwa mara zote kutosaidia kufungua simu za wateja wao.