Watu wengi hununua simu zilizotumika kwa mda (used phones) kutokana na hali ya kutomudu gharama kubwa za kununua simu mpya, japo kununua simu mpya ni vizuri zaidi ila kutokana na bei kuwa juu wengi huamua kusubiri ili wapate ambazo zimetumika kwa mda mfupi hasa simu za hali ya juu (high end smartphones).
unatakiwa kuwa mwangalifu sana pindi ununuapo simu iliyotumika, leo utajifunza vitu vya kukusaidia kufanya uamuzi bora.
1. Hali yake ya nje.
Jambo la kwanza la kuangalia wakati unanunua simujanja/smartphone iliyotumika ni hali yake ya nje, hali yake ya nje inakupa picha ya wazi namna gani simu imetunzwa na mtumiaji.
Angalia mikwaruzo au kama simu imepasuka, angalia kama vitufe/buttons zote zinafanya kazi kwa usahihi, angalia sehemu zingine zenye matundu/ports kama sehemu ya kuchajia, angalia na ujaribu ubora wa microphone, spika/speaker ili kujiridhisha. kingine angalia na ujaribu ubora wa kamera/camera na pia kagua uone kama lensi zake zimechubuka au ziko kwenye hali nzuri.
2. Angalia kama inaweza kutumika na mtoa huduma wako wa mtandao.
Unapaswa kununua kifaa kinachoweza kutumika vyema bila kuwa na shida kwenye suala la mtandao, kuna simu hasa za Android zinakuwa zimefungwa au zimezuiliwa kutumika baadhi ya maeneo kiasi kwamba haziwezi kupata mtandao kutoka kwa mtoa huduma wako, mfano ukiweka laini ya simu kama Vodacom, Tigo, Airtel n.k simu haiwezi kuonyesha mtandao yaani huwezi kupiga wala kupokea simu (Network Lock). kwahiyo unapaswa kununua simu inayoweza kuingiliana na mtandao wa sehemu husika ulipo.
3. Betri/Battery
Betri ni kifaa cha msingi sana kuangalia kwenye simujanja (smartphones) maana ndiyo kitu kinachoathirika zaidi kulingana na mda wa matumizi ya simujanja (smartphones). Kitu cha kuangalia ni afya ya betri ya simu yako (Battery health), kwa simu za iPhone ukifungia Mipangilio (settings), nenda mpaka kwenye sehemu ya Battery ukifungua hapo utaona Battery Health, kadri asilimia zikiwa kubwa ni ubora wa betri unakuwa mkubwa zaidi. Kwa simu za android utahitajika kupakua programu kama “Battery monitor”. Lakini unatakiwa ujue pia namna bora ya kutunza betri ya simu yako.
4. Je, simu imerekebishwa au imetumika bila kurekebishwa? (Is it Refurbished or Used?)
Unapokuwa kwenye soko la simu zilizotumika hasa upande wa Android, utakutana na vionjo viwili, simu zilizotumika kisha kurekebishwa au simu ambazo hazijarekebishwa.
Refurbished maana yake simu imetumika kisha ikarudishwa kiwandani kwa ajili ya matengenezo au maboresho na kisha kurudi tena sokini, mara nyingi hizi simu zilizotoka kwenye kiwanda cha mtengenezaji zinakuwa kwenye box na kifurushi(package) chake ni kama zilivyo simu mpya mfano warranty, na vifaa vingine kama chaja/charger n.k
Used ni simu iliyotumiwa na mtu, inatoka mkononi mwa mtu moja kwa moja, haipo kwenye boksi.
5. Uthibitisho wa ununuzi (Proof of purchase)
Jambo la muhimu la kuangalia unapotaka kununua bidhaa iliyotumika kwa kifaa chochote cha kielekroniki au la, ni uthibitisho wa kununuliwa, hakikisha unanua kwenye duka linaoaminika au kama ni mmiliki wa simu hakikisha unauliza risiti halali za mauzo kuhakikisha kama yeye ndiye mmliki halali wa kifaa. Hii itaepusha kununua kifaa kilichoibiwa.
Na pia utajua kama kifaa kipo kwenye dhamana/Warranty na kimetumika mda gani na kimepita kwenye mikono ya watu wangapi, vifaa vilivyotumika mara nyingi havina dhamana ni wewe kuchagua ununue kifaa kisicho na dhamana/warranty au la.
6. Sera ya kurudisha (Return policy)
Unaponunua kifaa kilichotumika hasa vifaa vya kielekroniki lazima ukubaliane na muuzaji endapo kifaa hakitofanya kazi kama inavyotakiwa basi unaweza kurudisha ubadilishiwe ama upewe pesa yako,
Sera ya kurudisha hufanya kazi kama dhamana/warranty endapo simu imeshindwa kufanya kazi ilivyotakiwa, japokuwa hii sera ya kurudisha ina mda mfupi sana kuliko dhamana/warranty ya kifaa kipya, sera ya kurudisha inaweza kuwa ni wiki mbili tu tangu umenunua kifaa.
7. Gharama.
Gharama ya simu iliyotumika hutegemea na vitu kadhaa kama hali yake, imezinduliwa lini, ukubwa wake n,k. unatakiwa pia kufanya utafiti wako kujua gharama za simu mbalimbali ikiwezekana uliza wataalamu au pitia mitandaoni kujua gharama za simu kwa wakati huo ili kuepusha kuuziwa simu kwa gharama kubwa au kutaka kitu cha gharama kubwa kwa bei ndogo ikapelekea ukapata kitu kibovu.
Jua nini cha kuangalia unaponunua simu iliyotumika (used smartphone)
Hayo ni baadhi ya mambo ukiyafata yatakusaidia kufanya ununuzi wako vizuri na kupata kifaa bora zaidi kwa pesa yako.
Kama una swali au maoni tuandikie tutakujibu.
No Comment! Be the first one.