Unaweza ukawa unajiuliza sana nap engine hata usiihusishe sana kampuni ya Apple na magemu (games) lakini ndio hvyo inategeneza hela nyingi tuu.
Katika Ripoti ambayo imetoka ya mwaka 2021 inaonyesha Apple ikipata mauzo ya juu kabisa ukilingnaisha na makampuni kama vile Microsoft, Activision na Nintendo.
Katika kipindi cha mwaka 2021 pekee kampuni ya Apple imeweza kupata mapato ya dola bilioni 15.3 katika maswala ya magemu pekee.
Kwa sasa Apple inamiliki jukwaa kubwa sana ambalo linajihusisha na maswala ya magemu katika simu.
Kumbuka mapato mengi yanatoka katika magemu yanayomilikiwa na wengine katika App Store.
Google na Apple inasemekana inachukua kati ya asilimia 15 mpka 30 ya manunuzi yote yanyofanyika ndani ya magemu ambayo yapo katika masoko yao.
Lakini kumbuka kwa mwaka huu mambo yanaweza yakabadilika sana kwani kampuni kama vile Sony imefanya ununuzi wa makampuni mengi
Microsoft na wenyewe na ununuzi wao wa Activision/Blizzard, hii inaweza badilisha matokeo hapo baadae maana kila mtu atataka afanye vizuri katika soko hili.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment. Je Ni Jukwa Kutoka Kampuni Gani Ambapo Unapenda Kucheza Magemu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.